Thursday, November 26, 2020

SINGIDA YAWANOA WANAUSHIRIKA

 

Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Singida, Thomas Nyamba akiongea na Waandishi wa Habari.

                  

Mwenyekiti wa   Chama Kikuu Cha Ushirika  cha Wakulima Mkoa wa Singida (SIFACU LTD) Yahaya Ramadhani  akiongea na Waandishi wa Habari


 Wajumbe wa Bodi na Watendaji wa   Vyama vya Ushirika  katika  Mkoa Singida  wakipewa mafunzo

                            ......................................

 

John Mapepele na Rose Nyangasa, Singida

Mkoa wa Singida umeandaa  mafunzo  ya siku  tatu ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa Bodi na Watendaji wa   Vyama vya Ushirika  katika  Mkoa ili kuwasaidia  kuacha  kufanya kazi kwa  mazoea  badala yake wafanye  kazi  kwa weledi na kwa kuzingatia sheria  huku wakitanguliza mbele maslahi ya wakulima. 

 

Akifungua mafunzo hayo leo mjini Singida kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia eneo la Uchumi Beatus Choaji amesema Mkoa umeamua kufanya  mafunzo hayo kutokana na kupata taarifa  ya ukaguzi uliofanywa kwenye vyama vya ushirika  kushindwa kufanya vizuri.

 

Choaji amesema Serikali ya Awamu ya Tano ipo macho kwa viongozi wa Vyama Vya Ushirika na maafisa wengine wa Serikali ambao wamekuwa wakishirikiana na walanguzi kuwanyonya wakulima ambapo amesema hili ni  kosa kisheria  na  kuwaonya kwamba  katika kipindi cha sasa Sheria kali zitachukuliwa dhidi yao ikiwa ni pamoja na kuwatia hatiani kwa Sheria ya Uhujumu Uchumi.

 

 “Nawaagiza Watumishi wa Serikali kuacha kufanya kazi kwa mazoea badala yake fanyeni kazi kwa weledi na kuzingatia Sheria huku mkitanguliza mbele maslahi ya wakulima”aliongeza Choaji

 

Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Singida, Thomas Nyamba amesema lengo la  kuandaa mafunzo hayo ni kutoa elimu  ya kuwawezesha Watendaji ili waweze kutekeleza majukumu yao kikamilifu.

 

Nyamba amesema kumekuwa na makosa mbambali ya kiuzembe  na kitaaluma katika utendaji wa kazi lakini kupitia mafunzo haya watendaji wote watabadilika.

 

Mwenyekiti wa   Chama Kikuu Cha Ushirika  cha Wakulima Mkoa wa Singida (SIFACU LTD) Yahaya Ramadhani  amesema pamoja na mambo mengine wajumbe wa kikao hicho watafundishwa masomo ya uandishi wa vitabu vya mwanzo na vitabu vikuu,uaandaaji wa taarifa za fedha,uongozi na utawala pia na Sheria ya Vyama Vya Ushirika Na.6. ya Mwaka 2013

 

Ameyataja masomo mengine yatakayo fundishwa kuwa ni uandaaji wamakisio ya mapato na matuminzi,uandaaji wa mpango mkakati, utatuzi wa migogoro na usimamizi wa fedha na udhibiti wa rushwa katika vyama vya ushirika.

 

Baadhi ya washiriki katika wa mafunzo hayo wamepongeza juhudi za Serikali ya awamu ya Tano kutoa mafunzo na kusema kwamba yataongeza tija katika utendaji wao wa kazi.

 

Mwenyekiti wa AMCOS wa Wilaya ya Ikungi Mnang’ana Rukia Jumanne amesema mafunzo hayo yamewasaidia kutambua majukumu ya kila mmoja kwenye vyama vya ushirika hivyo yatawawezesha kufanya kazi bila kuingiliana nakwa weledi tofauti na kipindi cha awali.

 

Naye Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Dkt. Rehema Nchimbi amesisitiza kwamba   kwa sasa Serikali imeweka  mikakati madhubuti ya kuufanya Mkoa wa Singida  kuwa miongoni mikoa itakayozalisha kwa  wingi mazao na  kuilisha Tanzania na nchi  mbalimbali za Afrika  na dunia kwa ujumla na hivyo kuwa na  Vyama vya Ushirika  makini ni jambo  lisiloepukika  kwenye Mkoa wa Singida.

“Tumeanza vizuri kwenye zao la Korosho na Alizeti sasa tunaongeza nguvu kufufua na kuanzisha mazao ya Mkonge na Parachichi” aliongeza Mhe. Nchimbi

Tuesday, November 10, 2020

TAKWIMU ZAIPAISHA TANZANIA UCHUMI WA KATI -SERIKALI

 


 A

A     Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Anjelina Lutambi (aliyesimama) akitoa ufafanuzi kwenye mkutano wa uelimishajiwa zoezi la ukusanyaji wa takwimu za mifugo,kilimo na uvuvi katika Kijiji cha  Msikii, Kata ya Muhamo, Mkoani Singida hivi karibuni(Pichana John Mapepele).

B

A.      Bibi Salma Mkumbo akiuliza swali kwa wataalamu kwenye mkutano wa uelimishaji wa zoezi la ukusanyaji wa takwimu za mifugo,kilimo na uvuvi katika Kijiji cha  Msikii, Kata yaMuhamo, Mkoani Singida hivi karibuni (Pichana John Mapepele).

c

A.      Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Dkt. Albina Chuwa (aliyesimama) akitoa ufafanuzikwenye mkutano wa uelimishaji wa zoezi la ukusanyaji wa takwimu za mifugo,kilimo na uvuvi katika Kijiji cha  Msikii, Kata yaMuhamo, Mkoani Singida hivi karibuni(Pichana John Mapepele).

DMeneja Takwimu Ofisi ya Taifa ya Takwimu Mkoa wa Singida, Naing’oya Kipuyo( aliyesimama) akitoa maelezo kwa  katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Anjelina Lutambi (mwenye miwani) na Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Dkt. Albina Chuwa (hayupo pichani) kwenye ofisi ya Serikali ya kijiji cha Msikii, Kata yaMuhamo, MkoaniSingidaHivikaribuni(Pichana John Mapepele).
E
Elibariki Musa, Mkazi wa kijiji cha Msikii Kata ya Muhamo, Mkoani Singida akiuliza swali kwa wataalamu  (Pichana John Mapepele)


Na John Mapepele, Singida 

Serikali imesema takwimu sahihi zilizokusanywa kutoka kwenye sekta mbalimbali za kimkakati za Mifugo, Kilimo na Uvuvi nchini zimeifanya Tanzania chini ya Uongozi wa Rais wa Awamu ya Tano Mheshimiwa John Pombe Magufuli kuingia kwenye Nchi za Uchumi wa Kati duniani.

Hayo yamesemwa hivi karibuni na ujumbe maalum wa kitaifa ulioongozwa na Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Dkt. Albina Chuwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Anjelina Lutambi wakati  walipokuwa wanakagua zoezi la kitaifa ya ukusanyaji taarifa za kina za Kilimo, Mifugo, ufugaji wa samaki Mkoani Singida ambalo  limekamilika  hivi karibuni kwa mafanikio makubwa.

“Madhumuni makuu ya Sensa hii ni kupata taarifa muhimu za kilimo, mifugo na uvuvi zitakazotumika katika kupanga na kutathmini utekelezaji wa mipango mbalimbali ya maendeleo ya sekta katika taifa la Tanzania, na endapo ukusanywaji wa takwimu utakuwa kwenye ubora unaositahili utasaidia kulifanya taifa kupea kwenye uchumi wa juu kabisa katika kipindi kifupi kijacho” ameongeza Dkt. Chuwa

 

Akifafanua amesema taarifa  kwa mfano za magonjwa ya mifugo na mazao zitaisaidia Serikali kuainisha maeneo yanayokabiliwa na visumbufu/magonjwa  ili kuchukua hatua stahiki na kupanga mipango ya kudhibiti.Pia taarifa kuhusu uzalishaji wa mazao zitasaidia kujua kiasi cha uzalishaji kwa maeneo husika na kuiwezesha Serikali kupanga upatikanaji wa masoko na uwezekano wa kuanzisha viwanda vya kusindika mazao hayo.

 

Aidha amesema taarifa kuhusu upatikanaji na matumizi ya ardhi zitatumika kupanga mipango ya matumizi bora ya ardhi vijijini  hivyo zitatumika kutatua migogoro ya wakulima na wafugaji hapa nchini.

 

Dkt. Chuwa ameongeza kuwa matokeo ya Sensa ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi yanatarajiwa kuweka msingi imara wa sekta hii kwa miaka mingi iyajo, kwa  kuwa Sekta ya Kilimo ina umuhimu mkubwa  kwenye mustakabali wa maisha ya binadamu kwa kuwa ndiyo chanzo cha chakula na malighafi zinazohitajika katika viwanda hususani katika awamu hii inayoongozwa na dira ya uchumi wa viwanda.

 

“Kutokana na umuhimu huo, na kupitia Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Dunia ya Mwaka 2030, Sekta ya Kilimo ilipewa Lengo la Pili  la Kutokomeza Njaa, Kuwa na Uhakika wa Chakula, Lishe Bora na Kukuza Kilimo Endelevu. Aidha, lengo hilo limesisitiza umuhimu wa kuongeza tija katika sekta ya kilimo kwa kuongeza thamani ya mazao na pia kusisitiza matumizi bora ya ardhi na kurutubisha udongo, ili kuongeza uwezo wa binadamu kukabiliana na kuhimili mabadiliko ya tabianchi na athari zake yakiwemo majanga mbalimbali kama mafuriko na ukame pamoja na majanga mengine ikiwemo ndege waharibifu” ameeleza Dkt. Chuwa

   

Dkt. Lutambi amesisitiza kuwa pamoja na faida za jumla ambazo mkulima atakazozipata Sensa hii itamsaidia mtu mmoja mmoja kutatua changamoto mbalimbali katika kilimo,mifugo na uvuvi hasa upatikanaji wa pembejeo, huduma za ugani, upatikanaji wa masoko kwa mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi.

Ameongeza kuwa takwimu ni kitu cha msingi katika kupanga maendeleo kuanzia kwenye ngazi ya kijiji hadi taifa kwa kuwa zinasaidia kuonyesha changamoto na mafanikio na hivyo kusaidia kupata ufumbuzi wa kudumu wa changamoto hizo.

“Ni muhimu tukafahamu kuwa takwimu sahihi za mifugo, mazao na uvuvi zitasaidia  uchangiaji wa malighafi za  viwanda  vyetu hivyo kukuza uchumi wetu ambao tunautaka wa viwanda” amesisitiza Dkt. Lutambi

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Mohamed Bashe, kwenye hotuba yake, wakati  wa ufunguzi wa mafunzo ya wadadisi wa Sensa ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ya Mwaka wa Kilimo 2019/20, iliyofanyika katika Ukumbi wa TMDA,Mwanza Julai, 25 mwaka huu alisisitiza Mwaka huu 2020, Benki ya Dunia imeitangaza Tanzania kuwa katika kundi la nchi zenye uchumi wa kipato cha kati, ambapo alisema Taarifa hizi zimeleta faraja kubwa kwa sekta ya kilimo  kwa kuwa ndiyo iliyotoa mchango mkubwa zaidi katika Pato la Taifa wa asilimia 26.6 mwaka 2019 na pia inatoa ajira kwa takribani asilimia 66 ya watu wenye uwezo wa kufanya kazi.

 

“Sekta ya kilimo ilichangia asilimia 24.3 ya mapato ya mauzo nje ya nchi mwaka 2019. Fedha hizi kwa kiasi kikubwa zinatumika nchini katika mambo mbalimbali ikiwemo ujenzi wa miundombinu wezeshi ya barabara, reli, maji, usambazaji umeme na kuimarisha miundombinu ya kutolea huduma za jamii kama vile afya na Elimu kwa lengo la kuimarisha maendeleo ya wananchi” alifafanua Dkt. Bashe

 

Aliongeza kuwa, kwa mujibu wa Ripoti ya Tathmini ya Umasikini Tanzania Bara ya Mwaka 2018, sekta hii ikiendelezwa vyema ndio pekee yenye uwezo wa kuleta maendeleo jumuishi nchini, hivyo  kuna umuhimu mkubwa wa zoezi la sensa ya mifugo, mazao na uvuvi likafanyika kwa ubora na kwa umakini  unaositahili.

 

Pia wakati wa tukio la uzinduzi wa mafunzo ya wadadisi wa Sensa hii, Mwenyekiti wa Bodi ya Usimamizi ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Amina Msengwa amesisitiza kuwa takwimu zina mchango mkubwa katika maandalizi na utekelezaji wa sera na mipango, na vile vile katika kufanya maamuzi sahihi yanayotakiwa kufikiwa kwa kutumia ushahidi stahiki (evidence based decision making).

 Amesema Sensa ya Mwaka wa Kilimo 2019/20, ni ya tano kufanyika hapa nchini tangu nchi ipate uhuru na inafanyika kwenye jumla ya maeneo yaliyochaguliwa ya kuhesabia2,820 ambapo kutokana na maeneo hayo kaya 33,807 kutoka Tanzania bara na Zanzibar.

Kwa upande wake, Meneja Takwimu Ofisi ya Taifa ya Takwimu Mkoa wa Singida, Naing’oya Kipuyo ameishukuru Serikali ya Mkoa wa Singida kwa kusaidia kufanikisha zoezi hili ambalo  limefanyika kwa takribani siku 50 ambapo pia amewapongeza wananchi kwa kutoa ushirikiano wa  kutosha.

 

 Kipuyo amesema taarifa zilizokusanywa kwenye Sensa hii ni za kipindi cha kuanzia tarehe 1 Oktoba, 2019 hadi tarehe 30 Septemba, 2020 na kuongeza kuwa Mkoa wa Singida umekamilisha zoezi hilo kwa maeneo yote ambapo maeneo madogo ya kuhesabia watu yaani Enumaration Areas (EA) 90 yenye kaya 1087 zilizochaguliwa kwa ajili ya kufanyiwa sensa hii zilifikiwa

Monday, November 9, 2020

WAFANYAKAZI WA BENKI YA I&M WAMEJITOLEA KUELIMISHA JAMII JUU YA MAMBO YA FEDHA NA UWEKAJI AKIBA KWA WANAWAKE NA VIJANA WAJASIRIAMALI

 

Timu ya wafanyakazi wa benki ya I&M waliovalia t-shirt za blue wakiwa katika picha ya pamoja na kikundi cha wanawake wajasiriamali kilichopo Yombo vituka walipoenda kutoa elimu ya bure kuhusu usimamizi wa fedha na ujasiriamali

Peter Joseph meneja msaidizi idara ya rasilimali watu akitoa elimu ya ujasiriamali kwa wanawake walioudhuria katika mafunzo hayo, Yombo jijini daresalaam.

Timu ya wafanyakazi wa benki ya I&M waliovalia t-shirt za blue wakiwa katika picha ya pamoja na kikundi cha wanawake wajasiriamali kilichopo Yombo vituka walipoenda kutoa elimu ya bure kuhusu usimamizi wa fedha na ujasiriamali

Mmoja wa wanawake walioudhuria katika mafunzo hayo, Bi. Eva Tumaini akizungumza na waandishi kuipongeza benki ya I&M kwa kutoa elimu ya fedha na ujasiriamali kwa jamii


Baadhi ya wafanyakazi wa benki ya I&M wakishirikiana na mmoja wa wanawake katika kufundisha mbinu za biashara ili kujikwamua kiuchumi kupitia mapishi.
 
                                                  ..................................................................
 


 Dar es salaam.

Benki ya I&M Tanzania yaanzisha mpango wa ‘IM FOR YOU’ ambao ni moja ya njia ya wafanyakazi wa benki hiyo kurudisha kwa jamii kwa kujitolea elimu bure kuhusu mambo mbalimbali ya kibenki ikiwemo maswala ya matumizi ya fedha, uwekaji akiba na ujasiriamali.

Siku ya Ijumaa Novemba 6, wafanyakazi wa Benki ya I&M wakiongozwa na Meneja Masoko na Mawasiliano ya Benki, Bi. Anitha Pallangyo, Meneja Msaidizi wa idara ya Rasilimali watu, Elimu na Maendeleo Bw. Peter Joseph, Bi. Hellen Mbwana kutoka idara ya ukaguzi wa ndani na wafanyakazi wengine waliotoka katika matawi ya hapa Dar es Salaam na idara nyingine mbalimbali ndani ya benki hiyo, walitembelea vikundi vya kina mama wajasiriamali wadogowadogo waliopo maeneo ya Yombo vituka jijini Dar es salaam, na kutoa elimu ya kuhusu mambo ya fedha, uwekaji akiba na ujasiriamali kwa wakina mama hao waliokusanyika kujipatia elimu hiyo.

Akielezea lengo la kuanzisha mpango huu wa ‘IM FOR YOU’ unaomaanisha ‘I&M Kwaajili yako’, wa kutoa elimu bure kwa jamii na lengo la kutembelea vikundi hivyo vya wakina mama vilivyopo maeneo ya Yombo Vituka, Bi. Anitha Pallangyo alisema, “Tumeazisha mpango huu kama moja ya njia ya kurudisha kwa jamii kile ambacho timu yetu ya rasilimali watu imekipata kutoka kwenye kazi zetu za kila siku, na kama tunavyojua kuwa elimu ni ufunguo wa maisha, hivyo tumeona ni vyema kukutana na vikundi mbalimbali vya wakina mama na vijana hasa ambao wanajishughulisha na biashara ndogondogo kujikwamua kiuchumi, ili kuwaongezea ujuzi na mbinu za kuongeza kipato. Mpango huu utasaidia hata serikali kupunguza idadi ya watu ambao hawajaajiriwa kwani unalenga kumfungua kijana na watanzania kwa ujumla kubuni mbinu mbalimbali za kibiashara ili kuweza kujiajiri.

Bw. Peter Joseph, Meneja Msaidizi idara ya rasilimali watu akiongea na waandishi katika tukio hilo alisema Benki ya I&M inajitahidi kuajiri wafanyakazi wenye uwezo mkubwa na ufanisi wa kazi, pamoja na kuwawezesha kuongeza ujuzi kupitia mafunzo mbalimbali ndani na nje ya ofisi hivyo imezalisha vijana wanaoweza kutoa elimu bora kwa jamii hasa kwa mambo ya fedha, umuhimu wa kujiwekea akiba na ujasiriamali.

Pamoja na kutoa elimu kwa jamii, timu hiyo ya wafanyakazi wa benki ya I&M ambayo ilienda kuwakilisha wafanyakazi wote kutoka idara mbalimbali, ilipeleka vitu mbalimbali ambavyo wafanyakazi walijitolea kwaajili ya kina mama wanaoishi kwenye mazingira magumu kama vile wajane, wamama wanaolea watoto yatima, na walemavu kwenye jamii hiyo, vitu hivyo ni pamoja na nguo, viatu, vyakula, sabuni, dawa za mswaki nakadhalka.

Benki ya I&M imekua mstari wa mbele katika kujitolea kwa jamii kupitia mikakati mbalimbali ya elimu, afya na mazingira. Benki hiyo inatoa huduma mbalimbali za kibenki kwa wananchi wote kwa ujumla ikiwemo akaunti za akiba za watoto, wanafunzi, wafanyabiashara, wanawake, mikopo, huduma za kuhamisha fedha, huduma za kubadili fedha za kigeni nakadhalika.  Benki hiyo inatarajia kuanzisha huduma za WAKALA hivi karibuni ambapo inategemea kuwa na  mawakala walioenea Dar es salaam na mikoani, pia ina matawi yanaoendelea kutoa huduma bora ambayo ni;Tawi la maktaba, tawi kuu linalo patikana mtaa wa Indira Gandhi, Kariakoo, Nyerere, Oysterbay, Moshi, Arusha na Mwanza. Pia kupitia huduma zake za benki kwa njia ya simu (Mobile Banking) *150*32#, kwa njia ya mtandao (Internet Banking) na App, wateja wake wanaweza kupata huduma za kibenki  saa 24 mahali popote wowote

Thursday, October 8, 2020

Benki ya I&M yasheherekea wiki ya huduma kwa wateja

 

 Wafanyakazi wa I&M Benki wakisherehekea pamoja na wateja maadhimisho ya wiki ya wateja huku wakiwa katika mavazi ya utamaduni ambapo siku ya Jumatano oktoba 7 ndio maadhimisho rasmi ya utamaduni wa Afrika.


Wafanyakazi wa I&M Benki wakisherehekea pamoja na wateja maadhimisho ya wiki ya wateja huku wakiwa katika mavazi ya utamaduni ambapo siku ya Jumatano oktoba 7 ndio maadhimisho rasmi ya utamaduni wa Afrika.
Wafanyakazi wa I&M Benki wakisherehekea pamoja na wateja maadhimisho ya wiki ya wateja huku wakiwa katika mavazi ya utamaduni ambapo siku ya Jumatano oktoba 7 ndio maadhimisho rasmi ya utamaduni wa Afrika.

Wafanyakazi wakiwa pamoja na wateja wa benki ya I&M siku ya Jumaatano ambapo benki hiyo iliadhimisha kilele cha Wiki ya Huduma kwa Wateja kwa kukata keki na wateja wao waliotembelea benki siku hiyo. Licha ya kukata keki pia benki ilichukua fursa ya kutembelea wateja wa kila ngazi, kutoa zawadi kama shukrani kwa wateja pamoja na kuvaa mavazi ya aina mbalimbali kuonyesha utofauti na furaha ya kuhudumia 

Wafanyakazi wa Benki ya I&M wakitoa zawadi kwa mteja wa benki hiyo kama moja ya njia ya kuwashukuru wateja kwa kuendelea kuitumia na kuiamini Benki ya I&M kwa huduma bora inazotoa kwa wateja wake na jamii kwa ujumla.


Wafanyakazi wa I&M Benki wakisherehekea pamoja na wateja maadhimisho ya wiki ya wateja huku wakiwa katika mavazi ya utamaduni ambapo siku ya Jumatano oktoba 7 ndio maadhimisho rasmi ya utamaduni wa Afrika.
Wafanyakazi wa Benki ya I&M wakiwa katika mavazi ya udaktari wakionyesha kuwapatia wateja suluhisho la changamoto za kifedha kwa kuwapatia wateja huduma bora kibenki ili kufanikisha shughuli za kibiashara na uchumi. Haya yote yamefanyika katika maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja 

Wafanyakazi wa Benki ya I&M wakiwa katika mavazi ya udaktari wakionyesha kuwapatia wateja suluhisho la changamoto za kifedha kwa kuwapatia wateja huduma bora za kibenki ili kufanikisha shughuli za kibiashara na uchumi. Haya yote yamefanyika katika maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja 
Mfanyakazi wa Benki ya I&M katika mavazi ya udaktari akiwa anatoa huduma kwa mmoja kati ya wateja waliotembelea tawi la benki hiyo katika maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja
 

                                                      ...........................................

Dar es Salaam

BENKI ya I&M Tanzania imeadhimisha Wiki ya Huduma kwa Wateja, kwa kutambua mchango muhimu unaotolewa na fanyakazi wake katika kuwahudumia wateja wao kwa viwango vya juu na kuhakikisha kuwa wanakuwa wenye furaha wakati wote.

Hafla hiyo ilifanyika leo maktaba square  jijini Dar es Salaam katika makao makuu ya benki hiyo, ikiambatana na shughuli mbalimbali kwa wateja kama ishara ya shukrani kwa wateja wanaothaminiwa na pia wafanyakazi wake ambao wamekuwa wakitekeleza jukumu muhimu la kutoa huduma bora kwa wateja wakati wote.

Miongoni mwa shughuli za kusherehesha hafla hiyo na wiki ya huduma kwa wateja zilizofanywa na benki hiyo ni pamoja na Maofisa wa juu na waandamizi wa benki hiyo akiwamo Afisa Mtendaji  Mkuu, walichukua jukumu la kuhudumia wateja katika matawi mbalimbali kwa siku ya leo.

Sheherehe hiyo ya wiki nzima ni matokeo ya kujitolea kwa benki hiyo ya I&M katika kuongeza ushiriki wa wafanyakazi katika kuunga mkono kaulimbiu ya mwaka huu ya siku hiyo inayosema kuwa, ‘Timu ya ndoto’.

Mbali na ushiriki wa watendaji wakuu, maafisa waandamizi katika kufanya jukumu la huduma kwa wateja, pia wafanyakazi wote wa benki hiyo walipokea barua binafsi za shukurani kwa bidii yao na kujitolea kwao katika kuleta matokeo chanya na furaha kwa wateja katika benki hiyo.

Mkuu wa Mauzo ya rejareja wa benki hiyo, Lilian Mtali alisema katika kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja wanataka onyesha thamani ya watoa huduma kwa wateja.

“Sisi benki ya I&M tunataka kutumia wiki hii ya huduma kwa wateja kuhakikisha kuwa tunawaonyesha thamani na ukarimu wateja wetu,lakini pia kuunga mkono na kutambua kazi nzuri na kubwa inayofanywa na maafisa wa huduma kwa wateja kama dawati namba moja ambalo ni nembo na kilelezo cha huduma bora za benki.

“Kwani sote tunatambua kuwa dawati la huduma kwa wateja ndilo limebeba sura na kilelezo cha huduma bora zinazotolewa na benki, wamekuwa wakaifanyakazi kwa bidi kwani hata pale wateja wanapokuwa na jazba, wao wamekuwa wakijitahidi kuhakikisha kuwa wanakamilisha mahitaji yao na kuwaacha wakiwa na furaha jambo ambalo ni kipaumbele cha benki,” alisema Lilian.

Wiki ya Huduma kwa Wateja ni maadhimisho ya umuhimu wa huduma kwa wateja na ya watu ambao wanahudumia na kusaidia wateja kila siku. 

Hafla hiyo huadhimishwa kila mwaka wakati wa wiki ya kwanza ya Oktoba na wafanyabiashara wote na mashirika yanayolenga huduma kote ulimwenguni, ambayo hutambua umuhimu wa kutoa huduma bora kwa wateja.

Wednesday, September 30, 2020

UN yamuunga mkono Magufuli kutokomeza ukatili wa mwanamke Ikungi

 

   Picha ya pamoja ya Mkuu wa mkoa wa Singida  Dk. Rehema Nchimbi(mwenye kilemba) na       wawakilishi wa mashirika ya kimataifa na wadau mbalimbali wa maendeleo mara baada ya uzinduzi wa mradi
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk Rehema Nchimbi(kulia) akiwa na Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa Nchini Tanzania, Zlatan Milisic baada ya kukata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa mradi
 

 Na John Mapepele, Ikungi
 MKUU wa  Mkoa wa Singida Mhe, Dk. Rehema Nchimbi  leo amezindua  miongoni mwa miradi mikubwa iliyowahi kutekelezwa nchini, mradi wa  pamoja  baina ya Mashirika ya Kimataifa ya UN Women na UNFPA kupitia ufadhiri  wa  Shirika la KOICA wa Tuufikie usawa  wa jinsia kupitia kuwawezesha wanawake na wasichana utakaogharimu takribani bilioni 11.5 za kitanzania  ambao utatekelezwa  katika Wilaya ya Ikungi mkoani Singida na Msalala mkoani  Shinyanga katika kipindi cha  miaka mitatu kuanzia sasa.
 Dk. Nchimbi amesema lengo kuu la mradi huo ni kuchangia  katika kuwawezesha  wanawake na wasichana  kuwakwamua kiuchumi na kijamii katika mikoa ya Singida na Shinyanga  ili kufikia usawa wa kijinsia ambapo amewataka watendaji wote wa Serikali ambao watatekeleza mradi huo kuwa makini katika utekelezaji wa mradi ili  malengo ya mradi huo yaweze kufikiwa.

Amesisitiza kuwa Serikali haitasita kuwachukulia hatua kali watendaji ambao  kwa namna moja au nyingine hawataendana na kasi ya utekelezaji wa miradi chini ya Serikali ya awamu ya Tano  inayoongozwa na Rais John Pombe Magufuli ambapo amesema  mrai huo  ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi  ili kuwaletea wananchi  maendeleo ya  kweli.

Kwa mujibu wa  Mkurugenzi wa  KOICA  Tanzania, Bi Jieun Mo,  walengwa wasio wa moja kwa moja takribani  wakazi 40,000 kutoka kwenye wilaya  ya Ikungi na Msalala na walengwa  wa moja  kwa moja 2350 wanawake na wasichana  kutoka katika wilaya hizo watanufaika na mradi huu ambapo pia  wanaume na wanawake 6000 wa Wilaya  ya Ikungi watanufaika kwenye eneo la muingiliano wa  hati za ardhi.

Mo ameainisha kuwa  shughuli za mradi katika kuwaweza wanawake  kwenye eneo la uchumi zitajikiza zaidi kwenye kuimarisha uwezo wa wanawake  na vijana   wakulima ili waweze kutumia  njia nzuri za kilimo na hali ya hewa katika uzalishaji wa alizeti na kilimo cha bustani, kukuza uuzaji wa pamoja, ujuzi wa ujasiriamali na wakala wa uchumi  wa wanawake  na kuimarisha  usalama wa ardhi na umiliki.

Amesisiza kuwa  shughuli hizo zitatekelezeka  kupitia kuunda  vikundi vya uzalishaji wa kilimo cha bustani kwa wanawake, kuunganisha  wanunuzi wa vikundi  vya wakulima vya wanawake,kusaidia ujenzi wa  ghala kubwa  moja la alizeti na kituo cha ukusanyaji kilomo cha bustani ili  kuboresha uuzaji wa pamoja na utunzaji baada ya kuvuna, kutoa mafunzo ya ujasiriamali, kutoa mafunzo ya ujasiriamali na ufikiaji wa habari za kifedha na kufuatilia ushauri wa usimamizi wa biashara na  fedha na kukuza  umiliki wa ardhi pekee na wa pamoja  wa wanawake kupitia utoaji wa  Hati za Haki za kimila za Makaazi(CCROs).

Mwakilishi wa UN Women  Bi, Hodan Addou ameishukuru Serikali  ya  Tanzania  kuwa ushirikiano wake katika kuhakikisha  kuwa mradi huu  hatimaye umeanza kutekelezwa ambapo amesema Shirika lake  linaunga mkono juhudi za Serikali za kumkomboa mwanamke ili kuondokana na  unyanyasaji wa kijinsia.

Bi Addou amesisitiza kuwa mradi utasaidia uwezeshaji kijamii kwa kuwawezesha  wanawake kusimamia haki zao, kujenga ujuzi wa ujasiiamali wa wanawake na wasichana kukabiliana  na unyanyasaji wa kijinsia na kuimarisha mifumo ya kuzuia na kukabiliana na unyanyasaji wa kijinsia kupitia kuanzisha na kuandaa vifaa katika madawati matatu ya  Polisi ya Jinsia na Watoto, kuanzisha  vituo vitatu vya  huduma  ya dharura katika  vituo vya wilaya, kuunda nafasi salama ya umma, kujenga uwezo  wa nambari ya msaada ya watoto kitaifa, kuunda na kuimarisha Klabu za Wasichana na kuunda Kamati za ulinzi na ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Kwa upande wake Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa Nchini Tanzania  Zlatan Milisic   ameipongeza Serikali kwa kuwa  na mradi huo na kuongeza kuwa mradi huo unaendana na malengo ya endelevu ya 2030 hususani lengo namba 5 kuhusiana kuwaendeleza wanawake  katika nyanja mbalimbali na kuongeza kuwa mwaka 2020 ni mwaka muhimu sana kwa kuwa tunaelekea  katika kutimiza miaka 25 ya azimio la wanawake la Beijing.

Ameeleza kuwa  malengo endelevu ya 2030 yameeleza kuwa ili kufikia maendeleo ya nchi kumtambua mwanamke ni jitihada muhimu sana  katika kuharakisha na kutimiza malengo yote ya maendeleo ambapo ameihakikishia Serikali ya Tanzania kuendelea kufanya kazi kwa karibu sana  ili kuhakikisha wanawake wanakuwa chachu ya maendeleo katika  nchi ya Tanzania.

Mwakilishi wa UNFPA, Dk. Winfred amesema kuwa uzinduzi wa mradi umelenga kutokomeza aina zote za unyanyasaji wa kijinsia  na kuimarisha usawa katika jamii ikiwa ni pamoja na  kuimarisha maisha ya wanawake ambapo amesisitiza kitovu cha matatizo ya kijinsia  ni wanaume na mila na desturi potofu zinazomtazama mwanamke kwa kumdharirisha hivyo juhudi za makusudi  zinatakiwa  kufanywa za kuwaweka wanaume mbele ili kutokomeza unyanyasaji wa kijinsia kwa wanawake.

Naye  Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Edward Mpogolo  amesisitiza kuwa kazi nzuri zinazofanywa na  Rais John Pombe Magufuli katika Nyanja mbalimbali ndiyo zinazoyafanya  jumuiya za kimataifa  kuunga mkono kwa kutoa  misaada  kupitia miradi mbalimbali hapa nchini

Thursday, September 17, 2020

BENKI YA I&M TANZANIA YAZINDUA KLABU YA MICHEZO KWA WAFANYAKAZI WAKE

 

Timu ya wafanyakazi wa I&M Benki walipozindua klabu yao ya michezo katika ofisi za makao makuu ya benki hiyo, Maktaba Square jijini Dar es salaam
Timu ya wafanyakazi wa I&M Benki walipozindua klabu yao ya michezo katika ofisi za makao makuu ya benki hiyo, Maktaba Square jijini Dar es salaam
Timu ya wafanyakazi wa I&M Benki walipozindua klabu yao ya michezo katika ofisi za makao makuu ya benki hiyo, Maktaba Square jijini Dar es salaam
 Timu ya wafanyakazi wa I&M Benki walipozindua klabu yao ya michezo katika ofisi za makao makuu ya benki hiyo, Maktaba Square jijini Dar es salaam

                                         ...............................................................................

Siku ya ijumaa tarehe 11 Septemba 2020, benki ya I&M Tanzania ilizindua klabu ya michezo kwaajili ya wafanyakazi wake kupitia kamati yake ya mabadiliko ya kitamaduni ambapo wamedhamiria kuongeza ari kwa wafanyakazi wake kwa njia ya michezo mbalimbali ikiwemo mbio fupi za riadha ambazo hufanyika kila wiki pamoja na michezo mingine kama vile gofu, mpira wa miguu, mpira wa kikapu na mpira wa mikono.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Mkuu wa kitengo cha wateja wa rejareja alisema, “Tumeamua kuanzisha klabu hii ili kuhamasisha wafanyakazi wetu kuwa na afya bora, kuchangamka kiakili na kuongeza mapato kwenye benki yetu kwani wafanyakazi watakua na uwezo maradufu wa kufikiria mbinu mbalimbali za kuongeza biashara.”

Viongozi wa klabu hiyo ambao ndio walisimama kidete kuhakikisha timu ya wafanyakazi imeweza kushiriki kikamilifu katika riadha ambayo ndio ilifungua dimba la klabu hiyo, Bi Anitha Pallangyo, Meneja wa masoko na mawasiliano wa Benki ya I&M na Bi. Juliana Mtei Meneja wa kitengo cha fedha walifurahia uzinduzi huo na kuongeza kuwa wana mipango mingi kupitia klabu hiyo kuhakikisha jina la Benki ya I&M linang’ara hasa kwa upande wa michezo.

Timu ya wafanyakazi wa Benki ya I&M wakiongozwa na Mkurugenzi wa benki hiyo Baseer Mohammed walifanya riadha fupi kutoka makao makuu ya benki hiyo kwenda viwanja vya coco beach pamoja na kurudi wakiwa wamevailia jezi za michezo za klabu hiyo ikiwa ni moja ya michezo ambayo imedhamiria kuimarisha afya za wafanyakazi.

Bw. Baseer Mohammed akiongea na mwandishi wetu alisema, “Najivunia sana kuwa na timu shupavu iliojaa vijana wenye nguvu na maarifa, pia wenye uthubutu wa kuipeleka benki kwenye levo nyingine kwa kuitangaza kupitia sekta ya michezo. Faida ya michezo kwa wafanyakazi ni pamoja na kuamsha ari ya kufanya kazi, kupunguza mawazo, kuongeza ufanisi wa akili, kuamsha timu pamoja na kuongeza mahusiano mazuri kazini.

Benki ya I&M pia imetajwa kuwa ni benki bora yenye nguvu nchini Kenya ambapo imeonekana ikiwa na fursa kubwa za ukuaji pamoja na kutengeneza faida zaidi. Benki ya I&M kwa sasa ipo Tanzania, Kenya (makao makuu), Rwanda, Mauritious (Bank One) na hivi karibuni Uganda